.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 8 Agosti 2017

WAKURUGENZI WA BARCELONA WAMFUATA PHILIPPE COUTINHO

Mchakato wa Barcelona kumuwania Philippe Coutinho umeongeza kasi baada ya leo asubuhi wakurugenzi wa klabu hiyo kuwasili Uingereza kujaribu kukamilisha mpango huo ili aweze kucheza dhidi ya Real Madrid jumapili.

Wakurugenzi hao wa Barcelona Oscar Grau, Raul Sanllehí na Javier Bordas wanatarajia kurejea Barcelona usiku wa leo wakiwa wamekamilisha mpango huo baada ya Liverpool kukubali kuwa Coutinho anataka kuondoka.

Timu ya Barcelona imeshatoa ofa ya paundi milioni 72 kwa Liverpool ili kumtwaa Coutinho wiki mbili zilizopita na ofa ya pili inayofikia paundi milioni 80 ambayo nayo imeshindwa kuwashawishi Liverpool.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni