Lionel Messi amefikisha magoli tisa
katika msimu huu, na ndio kwanza tupo mwezi Septemba, baada ya
kufunga magoli manne wakati Barcelona ikiichakaza Eibar kwa magoli
6-1.
Hii ilikuwa ni hat-trick yake ya
pili katika msimu huu, na goli lake la nne ni la 300 kuifungia
Barcelona tangu ahamie timu hiyo. Kwa ushindi huo Barcelona inaongoza La Liga kwa tofauti ya pointi tano.
Leonel Messi akifunga goli la kwanza kwa mkwaju wa penati
Kiungo wa zamani wa Tottenham, Paulinho akifunga goli la pili la Barcelona kwa mpira wa kichwa
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni