Mshambuliaji Romelu Lukaku amefunga
goli lake la sita katika Ligi Kuu ya Uingereza katika msimu huu na
kuipatia Manchester United ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Southampton.
Lukaku alitikisa nyavu katika dakika
20 ya mchezo kwa mpira uliogonga mwamba na kurudi baada ya kipa
Fraser Forster kupangua mpira wa kichwa wa krosi ya Ashley Young.
Kwa matokeo hayo Manchester United
wanaendelea na rekodi ya kutofungwa katika msimu huu na wapo nyuma ya
vinara Manchester City kwa tofauti ya magoli.
Mshambuliaji Romelu Lukaku akifunga goli pekee la Manchester United katika mchezo huo
Southampton walijaribu bila ya mafanikio kurejesha goli hilo ila kipa wa Manchester United alikuwa makini
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni