Timu ya Celtic imejikuta ikijuta
kuifahamu Paris St-Germain, baada ya kuchakazwa magoli 7-1 katika
mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya katika dimba la Parc de Princes.
Kikosi cha Brendan Rodgers kilikuwa
cha kwanza kufunga goli katika dakika ya kwanza kupitia kwa Moussa
Dembele, lakini goli hilo ilikuwa kama wamechokoza nyuki kwenye
mzinga.
Neymar alifunga mara mbili na
kutengeneza la tatu lililofungwa na Edinson Cavani, na kisha Kylian
Mbappe kufunga kabla ya mapumziko.
Marco Verratti, Cavani na Dani Alves
walifunga magoli ndani ya dakika tano katika kipindi cha pili na
kukifanya kikosi hicho cha Rodgers kupata kipigo cha magoli 7 kwa
mara ya kwanza.
Mshambuliaji nyota Mbrazil Neymar akiifungia PSG goli
Mfaransa Kylian
Mbappe akiwa amepiga mpira uliotinga wavuni
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni