.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 24 Novemba 2017

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TOKA TASWA

KAMATI ya Utendaji ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), iliyokutana Dar es Salaam hivi karibuni, imeteua wanahabari tisa kuunda Kamati ya Marekebisho ya Katiba ya chama. 

Wengi wa walioteuliwa ni wanachama wa TASWA na wengine ni viongozi wa zamani wa chama na pia baadhi ni wanahabari wa michezo.

Mwenyekiti wa kamati hiyo atakuwa ni Mwenyekiti wa zamani wa TASWA, Boniface Wambura ambaye licha ya kuwa mwanahabari pia ana taaluma ya sheria na kwa sasa ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi (TPLB) na Katibu wa Kamati atakuwa Wakili Emmanuel Muga.

Wajumbe ni Katibu Mkuu wa zamani wa TASWA, Abdul Mohammed wa gazeti la Mwananchi, Mhazini Msaidizi wa zamani wa TASWA ambaye kwa sasa ni Mhariri wa michezo wa gazeti la Daily News, Nasongelya Kilyinga.

Wajumbe wengine ni Florian Kaijage kutoka Azam Media, Mahmoud Zubeyri kutoka Bin Zubeiyr Blogs, Tunu Hassan wa EFM Redio, Benny Kisaka wa Jambo Concept na Majuto Omary wa gazeti la Citizen.

Hatua ya kuunda kamati hiyo inatokana na maelekezo kutoka Baraza la Michezo la Taifa (BMT), ambalo limetaka chama kifanye marekebisho ya katiba kwanza ili iwe rahisi kwa mambo mengine yafanyike katika utaratibu mzuri ikiwa ni pamoja na Uchaguzi Mkuu wa chama.

Kutokana na hali hiyo, Kamati ya Utendaji imekabidhi jukumu hilo kwa Kamati Maalum ambayo itapanga utaratibu wake wa namna ya kufanyia marekebisho katiba hiyo, ikimaliza itawasilisha rasimu ya Katiba kwenye Mkutano Mkuu wa chama kwa hatua nyingine.

Ni imani ya Kamati ya Utendaji kwamba Kamati ya Katiba inaweza kukamilisha rasimu hiyo katika muda usiozidi siku 90, ikiwa chini ya hapo itakuwa vizuri zaidi.

Tunaomba wadau wote tuipe ushirikiano wa namna mbalimbali kwa kadri itakavyowezekana ili tupige hatua katika kuimarisha chama chetu.

Nawasilisha,

Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA
24/11/2017

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni