.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 16 Februari 2017

DAKIKA 523 ZA CRISTIANO RONALDO UEFA BILA YA KUFUNGA GOLI

Cristiano Ronaldo amekuwa na wakati mgumu mno katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kukabiliwa na ukame wa kutofunga magoli kwa muda wa dakika 523.

Mchezaji huyo bora wa dunia amefunga magoli mawili tu katika michuano hiyo ya sasa, katika mchezo wa makundi dhidi ya Sporting Lisbon na Borussia Dortmund.

Ronaldo alishindwa kufunga jana wakati Madrid ikishinda magoli 3-1 dhidi ya Napoli katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora.
Cristiano Ronaldo akiwa chini akijaribu kumshawishi refa kuwa kachezewa rafu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni