.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 17 Februari 2017

KONGAMANO LA WANASAYANSI WATAFITI LAMALIZIKA JIJINI MWANZA

Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya Uchukuzi), Dkt Leonard Chamuriho (kushoto) akifuatiwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Prof. Faustine Kamuzora na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki wakishiriki Kongamano la Mazingira la Wanasayansi Watafiti wa Bonde la Ziwa Victoria lililomalizika jana jijini Mwanza.
Bi. Joyce Kasebela akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Bonde la Ziwa Victoria, ambaye pia ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge baada ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kuwa mmoja wa wadhamini wa Kongamano la Mazingira la Wanasayansi Watafiti wa Bonde la Ziwa Victoria lilimalizika jana jijini Mwanza.

Mwakilishi wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo wa Jijini Mwanza, Bi. Dorah Michael (kushoto) akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa Mhandisi Diana Munubi wa Mamlaka ya Viwanja vya ndege Tanzania (TAA) katika maonesho ya Washiriki wa Kongamano la Mazingira la Wanasayansi Watafiti wa Bonde la Ziwa Victoria jana jijini Mwanza.
Bw. Prenanning Pamer mkazi wa Mwanza akipata ufafanuzi wa masuala ya mazingira ndani ya viwanja vya ndege, kutoka kwa Mhandisi Diana Munubi kwenye maonesho ya washiriki wa Kongamano la Mazingira la Wanasayansi Watafiti wa Bonde la Ziwa Victoria, yaliyomalizika jana jijini Mwanza.
Bi. Joyce Kasebele wa Mamlaka ya Viwanja vya ndege Tanzania (katikati) akiwa na washiriki wenzake kwenye Kongamano la Mazingira la Wanasayansi Watafiti wa Bonde la Ziwa Victoria, lililofikia tamati jana jijini Mwanza.

Meneja wa Kiwanja cha ndege cha Jiji la Mwanza, Bi. Esther Madale (kulia) akiwa na Bi. Joyce Kasebele wa Kitengo cha Mazingira cha Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali katika Kongamano la Mazingira la Wanasayansi Watafiti wa Bonde la Ziwa Victoria. Kongamano hilo lilifanyika Jijini Mwanza.
ASP Andrew Majaliwa (kulia) akiwa ameshika moja ya vipeperushi vya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), baada ya kupata maelezo kuhusu mazingira kutoka kwa Mhandisi Diana Munubi kwenye maonesho ya washiriki wa Kongamano la Mazingira la Wanasayansi Watafiti wa Bonde la Ziwa Victoria, lililomalizika jana jijini Mwanza.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni