.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 17 Februari 2017

ZLATAN IBRAHIMOVIC ATUPIA HAT-TRICK NA KUIZAMISHA SAINT-ETIENNE

Zlatan Ibrahimovic amefunga magoli matatu yaani hat-trick wakati Manchester United ikianza vyema hatua ya 32 bora katika ligi ya Uropa na kuibuka na ushindi wa magoli 3-0 dhidi Saint-Etienne.

Ibrahimovic alifunga goli la kwanza kwa shuti la mpira wa adhabu uliogongwa na kumpoteza muelekeo kipa Stephane Ruffier, akafunga kiulaini tena mpira wa krosi ya Marcus Rashford, na kisha baadaye kupata penati ambayo nayo aliitumbukiza kimiani.

Mchezo huo ulitazamwa na Mama yake Pogba, Yeo na kaka yake Mathias ambao kama familia walikuwa wakishuhudia Pogba na kaka yake Florentin anayechezea Saint-Etienne wakichuana katika mchezo huo.
     Mpira uliopigwa na Zlatan Ibrahimovic ukielekea wavuni na kuandika goli la kwanza
Paul Pogba na Zlatan Ibrahimovic wakiangalia mpira wa kichwa uliopigwa na Pogba ukigonga mwamba
Paul Pogba akiongea na na kaka yake Florentin huku akizuia mdomo wake kwa mkono ili asiweze kutambulika anachomuambia

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni