.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 18 Machi 2018

TAGCO WAIKUMBUKA SHULE YA FAMILIA YA MZEE LAIBON ILIYOPO MTO WA MBU MKOANI MANYARA

Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusuano Serikalini (TAGCO) Pascal Shelutete akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Laiboni iliyopo Mto wa Mbu mkoani Manyara ,Rashid Mohamed msaada wa Madaftari 2500 kwa ajili ya wananfunzi wanaosoma katika shule hiyo.
Mwenyekiti wa TAGCO ,Pascal Shelutete na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji wa Serikali ,Dkt Hassan Abbas wakigawa Daftari kwa wanafunzi wanaosoma katika shule ya Msingi Loibon.
Mwenyekiti TAGCO ,Pascal Shelutete akizungumza mara baada ya kukabidhi Msaada huo.
Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusuano Serikalini (TAGCO) Pascal Shelutete akipeana mkono na Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Laibon ,Rashid Mohamed wakati akikabidhi msaaada wa Matenki mawili ya kuhifadhia maji shuleni hapo .kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari Maelezo.
Mwenekiti wa TAGCO ,Pascal Shelutete akizungumza jambo na Wanafunzi wanaosoma katika shule ya Msingi Loibon.
Moja ya majengo ya Shule ya Msingi Loibon iliyojengwa na Mfugaji wa Jamii ya Kimaasai,Loibon Ole Mapii baada ya Mungu kumjalia watoto Zaidi ya 200 na wajukuu Zaidi ya 400 na kulazimika kujenga shule kwa ajili ya familia yake.
Wenyeji wa eneo ilipo shule hiyo Jamii ya Wafugaji wa Kimasaai waliandaa Nyama kwa ajili ya ugeni uliotembelea shule hiyo.
Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Habari,Mawasilianona Uhusiano Serikalini (TAGCO) Pascal Shelutete na maafiwa Habar wenzake wakingojea kipande cha nyama . Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Arusha.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni