Ijumaa, 14 Machi 2014

WAMAREKANI SASA WAELEKEA BAHARI YA HINDI KUTAFUTA NDEGE ILIYOPOTEA

Mafisa wa Marekani wanaosaidia kutafuta Ndege ya Malaysia namba MH370, sasa wameelekeza nguvu zao katika eneo la bahari ya Hindi.
Hata hivyo afisa mmoja wa Marekani amesema hatua hiyo haina maana ya kuwa wamepata taarifa kuwa ndege imeanguka katika bahari hiyo.
Ndege hiyo ya Shirika la Ndege la Malaysia ikiwa na abiria 239 ilipotea siku ya Jumamosi, hadi sasa msako wake haujafanikiwa kuipata.
Waumini wa dini ya kiislamu wakiwa katika dua ya kuwaombea abiria waliopotea na ndege hiyo ya Malaysia toka siku ya jumamosi na mpaka leo kukosekana taarifa rasmi kama imeanguka au kutekwa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni