Meneja wa bia ya Serengeti Rodney Rugambo akiongea na mshindi wa kwanza
wa tiketi ya kwenda Brazil wakati wa droo ya nne ya promosheni ya Winda
Safari ya Brazili na Serengeti iliyofanyika mapema leo jijini Dar es
Salaam.
Akiongea kwa furaha iliyopita
kifani kwa njia ya simu mshindi wa kwanza wa tiketi ya kwenda Brazil Deusdedit
Kahwa kutoka Mbezi, Dares Salaam alisema alipata mshangao mkubwa sana kwa kuwa
hakutarajia kupata bahati hii ya kuwa mshindi wa tiketi na alishiriki
promosheni hii baada ya kuona matangazo yake kwenye televisheni.
Aliishukuru
Kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kumpa fursa
hiyo kubwa katika maisha yake na kuipongeza kwa kuwajali wateja wake kwa kuwapa
zawadi mbalimali zinogusa maisha yao. “nimefurahi sana na ninajiona mwenye
bahati sana kwa kushinda zawadi hii kubwa, hii ni mara ya kwanza kushinda
zawadi katika promosheni hii na nimepata zawadi kubwa sana na itakuwa ni mara
yangu ya kwanza kutoka nje ya nchi, nawashukuru sana Serengeti kwa kutujali
wateja wao” alimalizia Deusdedit
Meneja wa bia ya Serengeti Bw Rodney Rugambo alisema kuwa promosheni
hiyo ipo wazi kwa wanywaji wote wa bia ya Serengeti, na mpaka sasa kumekuwa na
washindi Zaidi ya 50000 waliojishindia bia za bure na pia zaidi ya washindi
2000 wa fedha taslimu kiasi cha shilingi 5000 na 10,000. Washindi
waliojishindia simu za Samsung tab katika droo ya leo ni Deo Msofe kutoka Kiboroloni,
Moshi na Jeremiah Ndelekwa kutoka Arusha. Pia wamepatikana washindi watano (5)
wa ving’amuzi ambao wote kwa pamoja watakabidhwa zawadi zao katika sherehe
maalum.
Nae Meneja Masoko wa
Kampuni ya Bia ya Serengeti Bw Allan Chonjo alisema “promosheni ya Winda Safari
ya Brazil na Serengeti bado inaendelea na tunapenda kuwakumbusha wateja wetu
kuwa hii ndio tiketi ya kwanza bado kuna tiketi nyingine na zawadi nyingine
nyingi zaidi, unaweza kufuatilia kupitia ukurasa wetu wa facebook www.facebook.com/serengetipremiumlager
kwa taarifa zaidi. Napenda kuwashukuru wateja wetu kwa kuendelea kutumia bidhaa
zetu na sisi tunawaahidi kuendelea kuwapa bidhaa zilizo bora na zenye viwango
na ubora wa hali ya juu”
Kunywa kistaarabu. Washiriki wanatakiwa kuwa na umri unaozidi
miaka 18. Vigezo na masharti kuzingatiwa.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni