Kiungo wa timu ya soka ya Arsenal, Jack Wilshere atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa majuma sita baada ya kuumia mguu wake wa kushoto. Mchezaji huyo aliumia mguu huo wakati alipokuwa akiwania mpira na Daniel Agger anayechezea Liverpool, katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliochezwa juzi kati ya Uingereza na Denmark. Katika mchezo huo Uingereza ilishinda bao 1-0
Jack Wilshere akiugulia maumivu makali


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni