Jumamosi, 8 Machi 2014

LIGI KUU UINGEREZA CHELSEA HAISHIKIKI, YAISAMBARATISHA BILA HURUMA TOTTENHAM MABAO 4-0

 Matajiri wa jiji la London, Chelsea hii leo wameendelea kujiimarisha kileleni katika msimamo wa ligi kuu Uingereza baada ya kuiangamiza Tottenham kwa mabao 4-0 katika mchezo ulioshuhudia vijana hao wa kocha msema hovyo Jose Mourinho wakiutumia vyeam uwanja wao wa nyumbani. 

Chelsea walijipatia mabao yao kupitia kwa Samuel Eto'o dakika ya 56, Eden Hazard dakika ya 60 kwa mkwaju safi wa penati na mtokea benchi Demba Ba akifunga mara mbili kunako dakika ya 88 na 89. Kwa matokeo hayo Chelsea wana pointi 66 na kuendelea kuongoza ligi kuu Uingereza wakifuatiwa na Liverpool walio nafasi ya pili na point 59
                Eto'o akiambaa ambaa uwanjani baada ya kuifungia timu yake bao
               Kaka chagua uende wewe au mpira, lakini mmoja abaki hapa
                       Younes Kabul wa Tottenham akizawadiwa kadi nyekundu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni