Jumapili, 9 Machi 2014

YANGA KUWAVAA WAARABU LEO BILA YA KIUNGO WAO NYOTA HARUNA NIYONZIMA

Kocha Mkuu ya timu ya Yanga, Hans Van Pluijm ametangaza kikosi kitakachowavaa Al Ahly hii leo huko Alexandria nchini Misri, bila ya kuwa na kiungo wao machachari Haruna Niyonzima.

Kwa mujivu wa taarifa kutoka kwenye kambi ya timu hiyo huko Misri Niyonzima atashindwa kushuka dimbani kuwavaa waarabu hao kutokana na kuugua ugonjwa wa malaria.

Katika mchezo wa awali uliochezwa Jijini Dar es Salaam timu ya Yanga iliibuka kidedea kwa kuifunga Al Ahly bao 1-0 na hii leo inakabiliwa na kibarua kigumu ya kuitoa timu hiyo katika Ligi ya Klabu Bingwa Afrika na kutinga hatua ya 16 Bora.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni