.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 23 Februari 2014

RAIS ROBERT MUGABE ASEMA NI AIBU KWA VIONGOZI WA AFRIKA KUTOMUENZI MWALIMU NYERERE

                                      Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere


Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ameeleza kuwa ni aibu kwa viongozi wa bara la Afrika kushindwa kumuenzi Baba wa Taifa la Tanzania Mwalimu Julius Nyerere kwa kujitolea kwake katika kukomboa bara la Afrika.

Rais Mugabe ametoa kauli hiyo jana katika hafla ya kutimiza miaka 90 ya kuzaliwa kwake iliyoandaliwa na Ikulu mara baada ya kurejea kutoka Singapore alipoenda kufanyiwa upasuaji wa jicho lake.

Rais Mugabe amewataka viongozi wa bara la Afrika kuongeza jitihada zaidi za kumuenzi Mwalimu Nyerere ambaye aliigeuza nchi yake kuwa kitovu cha harakati za ukombozi wa nchi za bara la Afrika.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni