.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 9 Machi 2014

NDEGE YA MALAYSIA BADO YAENDELEA KUTAFUTWA, HAKUNA TAARIFA ILIYOTELEWA MPAKA SASA KAMA IMEANGUKA AU LA, ILIKUWA NA ABIRIA 239

 Msako mkali umeendelea baharini kati ya Malaysia na Vietnam kutafuta ndege ya shirika la ndege la Malaysia Airline iliyopotoea toka imeondoka mjini Kuala Lumpar kuelekea Beijing nchini China. Ndege hiyo Boeng 777 ilikuwa na abiria 239, na ilipoteza mawasiliano masaa mawili baada ya kuruka
 Uchunguzi mkali umekuwa ukifanyika baharini kuangalia kama ndege hiyo ilianguka, na taarifa zinasema kuwa maofisa wa Vietnam wamesema wameona michirizi mikubwa ya mafuta katika bahari nje ya mwambao kusini mwa nchi hiyo, taarifa ambayo inaweza  kutafsiriwa kuwa ndege hiyo ilianguka baharini, japo bado taarifa hizo hazijathibitishwa na upande wowote
Marekani nayo imejitokeza kusaidia uchunguzi wa kuitafuta ndege hiyo baada ya kutoa meli yake ya kijeshi ili isaidie katika uchunguzi huo kama inavyoonekana pichani juu. Rweyunga Blog tunaendelea kuifuatilia taarifa hii kwa ukaribu na tutawajulisha wasomaji wetu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni