Jumapili, 9 Machi 2014

RADA YAONYESHA NDEGE ILIYOPOTEA ILIGEUZA SAFARI NA KUREJEA ILIPOTOKA

   Ndugu wa abiria aliyekuwemo kwenye ndege iliyopotea akiangua kilio uwanjani.
Rada imeonyesha kuwa ndege ya Shirika la Ndege la Malaysia ambayo imepotea kwa zaidi ya saa 24, huende iligeuza safari yake na kurejea ilipotoka.

Timu ya uokoaji imekuwa ikizidisha jitihada za kutafuta ndege hiyo kwa kuongeza upana wa eneo la zooezi hilo.

Wachunguzi pia wanaangalia picha za CCTV zinazoonyesha abiria wawili ambao wanaaminika wamepanda ndege hiyo kwa kutumia pasi za wizi.

Ndege hiyo MH370 ikitokea Kuala Lumpur kwenda Beijing ilitoweka angani Kusini mwa Vietnam ikiwa na abiria 239.
                          Msako wa angani ukiendelea kuitafuta ndege iliyopotea

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni