Alhamisi, 13 Machi 2014

RAIS WA BAYERN MUNICH AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MITATU JELA

Mahakama nchini Ujerumani imemhukumu Rais wa Klabu Bingwa Barani Ulaya ya Bayern Munich kifungo cha jela miaka mitatu na miezi sita kwa kukwepa kodi.

Rais huyo Uli Hoeness alikiri kufanya udanganyifu wa kodi kwa mamlaka ya kodi ya Ujerumani na kujilimbikizia mamilioni ya euro.

Hoeness ambaye alikuwemo kwenye kikosi cha Ujerumani kilichotwaa kombe la dunia, alificha fedha hizo kwa siri kwenye akaunti ya benki moja ya nchini Swiss.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni