Jumapili, 9 Machi 2014

WATU WANANE WAFA KATIKA AJALI ILIYOHUSISHA MAGARI MATATU NCHINI KENYA

Watu wanane wamekufa huku wengine wengi wakijeruhiwa baada ya magari waliyokuwa wakisafiria kugongwa na Lori kwenye barabara Kuu ya Nakuru-Eldoret alfajiri ya leo.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Polisi wa Kituo cha Rongai Joseph Mwamburi magari hayo ambayo ni basi la Matatu aina ya Nissan, Toyota Probox na Lori yalikuwa yakielekea Nakuru ambapo breki za Lori zilishindwa kufanya kazi na kuyagonga magari hayo mawili.

Abiria saba waliokuwamo kwenye basi la Matatu pamoja na mmoja aliyekuwemo kwenye Lori walikufa papo hapo huku majeruhi wengine wengi wakikimbizwa kwenye hospitali ya Nakuru.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni