.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 26 Mei 2014

WANAJESHI WAWILI WA KENYA WAUWAWA KWA KUPIGWA RISASI NA AL SHABAAB HUKO MOMBASA

Wanajeshi wawili wa Kikosi cha Ulinzi cha Kenya (KDF) wamepigwa risasi na kufa katika shambulio lililofanywa na wapiganaji wanaoshukiwa kuwa wa al Shabaab katika eneo la Kiunga, huko Lamu kwenye mpaka wa Kenya na Somalia.

Wanajeshi hao walijibu mashambulizi na kufanikiwa kumuua mmoja wa washambuliaji huku wengine wakifanikiwa kutoroka kwenye tukio hilo lililotokea jumapili jioni, ambapo wanajeshi wengine wawili walijeruhiwa.

Maafisa wa Jeshi la Ulinzi la Kenya, limesema wanajeshi hao walikuwa kwenye gari aina ya Land rover wakipita eneo la Milimani na ndipo gari lao lilipokwama kwenye tope na walipokuwa wakijaribu kulisukuma gari lingine lilifika na kuanza kuwashambulia kwa risasi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni