.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 13 Januari 2015

BALLON D'OR KWA MWAKA 2014, RONALDO AMFUNIKA KWA MARA NYINGINE MESSI

Mchezaji wa timu ya taifa ya Ureno na klabu ya soka ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo ( pichani juu ) kwa mara nyingine tena amembwaga mpinzani wake mkubwa, mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ajentina na FC Barcelona ya Hispania, Lionel Messi baada ya usiku wa kuamkia leo kutangazwa kuwa mwanasoka bora wa mwaka 2014 wa FIFA, maarufu Fifa Balon D'Or. 

Katika kinyang'anyiro hicho kilichofanyika mjini Zurich, Uswisi, Ronaldo alikuwa anachuana na Messi pamoja na mlinda mlango mahiri wa timu ya taifa ya Ujerumani na klabu ya Bayern Munich, Manuel Neuer.
Ronaldo akiiangalia tuzo yake baada ya kukabidhiwa na mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Ufaransa, Thierry Henry.

Wolfsburg's German midfielde Nadine Kessler ( katikati ) akizungumza machache baada ya kukabidhiwa tuzo ya mchezaji bora wa kike kwa mwaka 2014 wa FIFA.

Tuzo ya kocha bora wa mwaka 2014 wa Fifa alikwenda kwa Joachim Low toka Ujerumani.
Rais wa Shirikisho la soka ulimwenguni FIFA, Sepp Blatter akizungumza wakati wa utoaji wa tuzo hizo mjini Zurich.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni