.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 24 Januari 2015

FAINALI ZA MATAIFA AFRIKA 2015, ASAMOAH GYAN AIBEBA GHANA DAKIKA ZA MAJERUHI DHIDI YA ALGERIA

Timu ya soka ya taifa ya Ghana jana ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Algeria katika mchezo wa kundi C wa kuwania kombe la Mataifa Afrika, fainali ambazo zinaendelea nchini Equatorial Guinea. 

Katika mchezo huo, Ghana ilibidi wasubiri hadi dakika za majeruhi ndipo mshambuliaji wake mahiri Asamoah Gyan alipoifungia bao hilo muhimu katika dakika ya 90 ya mchezo. 

Kwa matokeo hayo, Ghana ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 3 nyuma ya Senegal yenye pointi 4 ikiwa ndio kinara wa kundi C. 

Nafasi ya tatu wapo Algeria wakiwa na pointi 3 na mkiani wapo Afrika Kusini wenye pointi 1.
Kocha wa Ghana, Avram Grant akimpongeza Asamoah Gyan baada ya kuifungia timu yake bao muhimu dhid ya Algeria hiyo jana.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni