.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 21 Januari 2015

FAINALI ZA MATAIFA AFRIKA 2015, IVORY COAST YALAZIMISHWA SARE NA GUINEA HUKU GERVINHO AKIPEWA KADI NYEKUNDU

Timu ya soka ya taifa ya Ivory Coast imeanza vibaya kjampeni za kuwania kombe la Mataifa ya Afrika zinazofanyika nchini Equatorial Guinea baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Guinea katika mchezo wa kundi D hapo jana. 

Katika mchezo huo, Ivory Coast waliokuwa chini ya nahodha Yaya Toure walilazimika kucheza wakiwa 10 uwanjani baada ya Gervinho kupewa kadi nyekundu kutokana na kitendo chake cha kumpiga kofi mchezo wa Guinea katika dakika ya 58 ya kipindi cha pili cha mchezo huo.
Guinea ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Naby Yattara katika dakika ya 36, bao ambalo lilidumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika. 

Kipindi cha pili ndipo Ivory Coast walipofanikiwa kupata bao la kusawazisha lililofungwa na Doumbia katika dakika ya 72 ya mchezo.
Mashabiki wa Guinea wakiishangilia timu yao ilipokuwa inacheza na Ivory Coast,

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni