.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 23 Januari 2015

FAINALI ZA MATAIFA YA AFRIKA, TUNISIA YAITANDIKA ZAMBIA 2-1 KWA MBINDE

Timu ya soka ya taifa ya Tunisia ilibidi ipigane kufa na kupona uwanjani na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Zambia katika mchezo wa kundi B wa kuwania kombe la Mataifa Afrika. 

Katika mchezo huo, Zambia ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 59 ya kipindi cha pili, bao lililofungwa na Emmanuel Mayuka. 

Timu zote zilionekana kutandaza soka safi na Zambia kuwa wanafanya mashambulizi ya kushtukiza langoni mwa Tunisia. 

Hata hivyo dakika ya 70 Tunisia walifanikiwa kupata bao la kusawazisha likifungwa na Ahmed Akaichi na baadaye Yasine Chikhaoui akaipatia Tunisa bao la pili nala ushindi katika dakika ya 88. 

Kwa matokeo hayo Tunisia ndio vinara wa kundi hilo wakiwa na pointi 4.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni