Penati hiyo ilitokana na nahodha na beki wa Manchester City, Vicent Kompany kumchezea madhambi Nacho Monreal ndani ya eneo la hatari.
Bao la pili la Arsenal lilifungwa na Olivier Giroud katika dakika ya 67 na kuizamisha kabisa Manchester City.
Kwa matokeo hayo, Arsenal wamefikisha pointi 39 wakiwa nafasi ya tano, huku Manchester City wakiendelea kubaki nafasi ya pili wakiwa na pointi 47, pointi 5 nyuma ya vinara wa ligi hiyo Chelsea.



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni