Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Wafanyabiashara nchini, Johnson Minja amefikishwa leo katika mahakama
ya Wilaya ya Dodoma akikabiliwa na mashtaka mawili ya kuwachochea
wafanya biashara wa mkoa wa Dodoma kutenda kosa na kuwazuia
wafanyabiashara hao kulipa kodi kwa kutumia mashine za kieletroniki
za Efds.
Akisoma mashtaka hayo mbele ya
Hakimu Mkazi wa mahakama ya Mkoa wa Dodoma, Rebeka Mbilu, mwendesha
mashtaka wa serikali Godfrey Wambali ameiambia mahakama hiyo kuwa
mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo Septemba 6, mwaka jana katika
ukumbi wa chuo cha mipango kilichopo Mjini hapa.
Wambali amesema katika kosa la
kwanza mshtakiwa alitenda kosa la jinai kinyume na kifungu cha sheria
namba 390 kinachokwenda sambamba na kifungu cha 35 cha kanuni za
adhabu sura ya 16.
Ambapo katika kosa la pili
mshatakiwa alitenda kosa kinyume na sheria kifungu cha 107c cha
sheria ya kodi sura ya 332 ya mwaka 2014.
Hata hivyo mshtakiwa alikana makosa
yote mawili na alirudishwa rumande baada ya kukosa wadhamini wawili
ambao walitakiwa kuwa na dhamana ya mali ya sh. 4 milion za mali
zisizohamishika ikiwa ni pamoja na mmoja wa wadhamini hao kuwa ni
mfanyakazi wa serikali.
Baada ya kushindwa kutimiza masharti
hayo, Hakimu Mbilu aliamuru mshtakiwa kurudishwa rumande hadi hapo
dhamana yake itakapokamilika. Kesi hiyo itatajwa tena Februari 11
mwaka huu.
Mwisho

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni