Mwili wa mfalme wa Saudi Arabia
Abdullah bin Abdulaziz umebebwa na kuingizwa katika msikiti uliopo
Riyadh, leo majira ya mchana, ikiwa ni chini ya saa 24 baada ya
kufariki dunia.
Mwili huyo ulikuwa umevingirishwa
kwenye kitambaa, wakati ukiingizwa kwenye msikiti mkubwa wa Riyadh wa
Turki Bin Abdullah ukiwa kwenye machela.
Mfalme huyo alifariki usiku wa
kumkia leo akiwa na umri wa miaka 90, akisumbuliwa na nimonia,
atazikwa kwenye kaburi lisilo na alama hii leo, kulingana na tamaduni
za Kiislam.
Taifa la Saudi Arabia lipo katika
maombolezo, huku makumi kwa maelfu ya watu wakikusanyika Jijini
Riayadh na Mecca kutoa heshima zao za mwisho.
Mwili wa mfalme wa Saudi Arabia
Abdullah bin Abdulaziz ukiingizwa msikitini



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni