Maafisa watatu mmoja wa Shirika la
Umeme Tanzania (TANESCO) na Mamlaka ya Mapato (TRA) pamoja na wa
Benki Kuu ya Tanzania (BOT) wamefikishwa leo Mahakamani Hakimu Mkazi
Kisutu kuhusina kashfa ya akaunti ya Tegeta Escrow.
Waliofikishwa mahamama hiyo leo Jiji
Dar es Salaam, Mwanasheria wa Tanesco Stephen Urassa, Afisa Misamaha
ya Kodi TRA Kyabukoba Mutabingwa na Mkurugenzi wa Fedha BOT Julius
Angelo, ambao wote wanatuhumiwa kuchukua rushwa ya fedha za
akaunti ya Escrow.
Katika kesi hiyo iliyoletwa na
Taasisi ya Kusuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) Urasa anashtakiwa kwa
kuchukua rushwa ya shilingi milioni 161.7, Angelo anashtakiwa
kuchukua rushwa ya shilingi milioni 161.7 na Mutabingwa kwa kupokea
shilingi bilioni moja na laki sita.
Mtuhumiwa Stephen Urassa ametoka nje
kwa dhamana wakati wenzake Kyabukoba Mutabingwa na Julius Angelo
wamepelekwa rumande baada ya kushindwa masharti ya dhamana.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni