.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 28 Januari 2015

WAZIRI MKUU WA JAPAN ALAANI VIDEO MPYA YA IS INAYOTISHIA KUMUUA RAIA WAKE

Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe amesema video mpya ya Dola ya Kiislam (IS) inayotishia kumuua mateka Kenji Goto ndani ya saa 24, inapaswa kulaaniwa na kukemewa.

Katika picha ya video sauti inayoaminika kuwa ni ya Goto raia wa Japan, inasikika ikisema yeye na rubani wa Jordan, watauwawa iwapo Jordan haitomuachia mwanamke wa Irak aliyehukumiwa kifo.

Bw. Abe amesema nchi ya Japan inashirikiana na nchi ya Jordan ili kufanikishwa kuachiwa kwa raia hao wao wawili.

Siku ya jumapili IS ilisema imemua raia mwingine wa Japan, Haruna Yukawa, baada ya dai lau la kupatiwa dola milioni 200, ili wamuachie kushindikana.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni