.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 8 Oktoba 2015

MATAIFA MATATU YA AFRIKA MAGHARIBI YAMALIZA WIKI BILA MGONJWA WA EBOLA

Mataifa matatu ya Afrika Magharibi ambayo yalikuwa yakikabiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola, yamekamilisha wiki moja bila ya kuwa na mgonjwa yeyote wa ugonjwa huo ulioanza mwaka 2014.

Mlipuko wa ugonjwa huo hatari umeuwa watu 11,000 katika mataifa ya Guinea, Liberia pamoja na Sierra Leone, kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO).

Matukio ya kesi mpya za wagonjwa wa Ebola yameshuka mno mwaka huu, hata hivyo shirika la WHO limeonya ugonjwa huo unaweza ukalipuka tena.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni