.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 3 Februari 2016

CFAO MOTORS YAFANYA ONYESHO LA BIASHARA YA MAGARI AINA YA SUZUKI KATIKA JENGO LA PSPF GOLDEN JUBILEE TOWERS

DSC_2617 
Moja ya Suzuki Grand Vitara magari ya CFAO yaliyopo kwenye maonyesho ya bidhaa mpya walizonazo katika jengo la PSPF Golden Jubilee Tower lililopo Posta jijini Dar es Salaam.
DSC_2588
                                            Gari hilo la Suzuki Vitara linavyoonekana kwa nyuma.
DSC_2592
                             Gari hilo aina ya Suzuki Grand Vitara linavyoonekana ubavuni.
DSC_2580
Moja ya Suzuki magari ya CFAO yaliyopo kwenye maonyesho ya bidhaa mpya walizonazo katika jengo la PSPF Golden Jubilee Tower lililopo Posta jijini Dar es Salaam.
DSC_2584
                                                Gari hilo la aina ya Suzuki linavyoonekana ubavuni.
DSC_2561
                                                               Suzuki hiyo inavyookena upande wa nyuma.
DSC_2575
                                                      Gari ndogo Suzuki OMNI inavyookena kwa mbele.
DSC_2600
Upande wa ndani unaogawa gari hilo la Suzuki ambao unaonesha upande wa dereva na upande ambao mtu anaweza kutumia kwa kuweka mizigo na mambo mengine.
DSC_2597
                               Upande wa nyuma wa ndaniu wa gari hilo aina Suzuki OMNI.
DSC_2602 
Magari hayo yanavyoonekana katika showroom hiyo ndani ya jengo la PSPF Golden Jubilee Towers.
 

Kampuni ya uuzaji magari ya CFAO imefanya onyesho la kuonyesha bidhaa mpya walizonazo katika jengo la PSPF Golden Jubilee Tower lililopo Posta jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Modewji Blog, Meneja Masoko wa CFAO Motors, Sheikha Said amesema sababu ya kampuni hiyo kufanya onyesho katika jengo hilo ni kuwaonyesha wateja wa kampuni hiyo bidhaa mpya walizonazo katika sehemu zao wanazouzia magari (showroom).

Amebainisha kuwa, mbali na kuwaonyesha wateja lakini pia kuwaonyesha wafanyakazi na wananchi mbalimbali ambao walikuwa hawajui bidhaa zinazopatikana CFAO Motors au kwa wengine kuwa na shughuli nyingi hivyo kushindwa kufika katika ‘showroom’ zao na kupitia onyesho hilo wataweza kupata magari katika maeneo yao ya kazi.

“Tupo hapa kwa hili kuwasogezea huduma watu wa aina mbalimbali na wafanyakazi wa taasisi mbalimbali waone bidhaa tulizonazo,” alisema Bi. Said.

Nae Afisa Mauzo wa Suzuki, David Kritsos alisema kupitia onyesho hilo wananchi na wafanyakazi wa ofisi mbalimbali wanaweza kununua magari wanayopendelea na wanaweza kusaidiwa na CFAO Motors kupata mkopo benki ili waweze kupata fedha za kununua magari hayo na kulipa mkopo taratibu.

Alisema CFAO ndiyo kampuni pekee nchini yenye nafasi ya kusambaza bidhaa za Suzuki na magari yote wanayoyauza bado ni mapya yakiwa bado hayajatumika kabisa.

Showroom hiyo itaendelea hadi hapo 4 Februari.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni