.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 3 Februari 2016

SIDA WARIDHISHWA NA MIRADI YA REA

2
Mtambuzi wa miradi kutoka Wakala wa Nishati Vijini, Mhandisi Elneema Mkumbo akitoa maelezo juu ya utekelezaji wa miradi ya REA, kwa Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Sweden( SIDA) Maria Van Berlokom ( aliyeweka mikono kifuania) ambao ni miongoni mwa wafadhili wa miradi hiyo akiwa na ujumbe wake pamoja na wadau wengine wa maendeleo ikiwemo Shirika la Maendeleo la Ujerumani( GIZ) wakati wakikagua utekelezaji wa miradi ya REA katika mikoa ya kanda ya kaskazini.
1
3 4
5
Muonekano wa nyumba zilizounganishwa na huduma ya umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati vijijini REA katika kijiji cha Kwedizinga mkoani Tanga.
 

                                                                                                  Na Mwandishi Wetu

Shirika la Kimataifa la maendeleo la Sweden( SIDA), limeridhishwa na utekelezaji wa miradi ya Umeme inayofahiliwa na Shirika hilo hususan usambazaji wa umeme vijijini unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini REA kwa kushirikiana na Shirika la Umeme nchini( Tanesco), katika maeneo mbalimbali nchini.

Mkuu wa Shirika la Kimataifa la maendeleo la Sweden( SIDA) Maria Van Berlekom amesema hayo mara baada ya kuona maendeleo ya wananchi wa vijijini wakati wa ziara yake ya kutembelea utekelezaji wa miradi hiyo katika mikoa ya kanda ya kaskazini .

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni