.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 6 Juni 2016

MKUTANO WA ACT WAZALENDO VIWANJA VYA ZAKIEM MBAGALA JANA JUMAPILI

Kiongozi mkuu wa cha upinzani nchini Tanzania ACT WAZALENDO ambaye pia ni mbunge wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama hicho jimbo la Kigoma Mjini Mh ZITTO KABWE akiwahutubia mamia ya wakazi wa jiji la Dar es salaam katika mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Viwanja Vya Zakiem Mbagala,mkutano ambao ulikuwa na lengo la Kuwaeleza watanzania hali halisi ya kile ambacho kimetokea katika bunge la Tanzania na kufanya Mbunge huyo na wenzake saba wa vyama vya upinzani kusimamishwa kuingia bungeni kwa vipindi tofauti.

Akizungumza katika mkutano huo ambao umetumika kama uzinduzi wa harakati za kuzunguka nchi nzima kudai Democrasia ambayo ameeleza kuwa imeanza kuminywa na serikali ya awamu ya Tano Mbunge huyo amesema kuwa Chama cha ACT WAZALENDO kimesema wazi kuwa kitamuunga mkono Rais wa Tanzania Dk JOHN MAGUFULI katika harakati zake za kupambana na Rushwa lakini kitampinga kwa nguvu zote katika harakati zake za kuiminya Deocrasia ya nchi.

Amesema kuwa Hatua ya wabunge saba wa Bunge la Tanzania kusimamishwa kuingia bungeni kwa kisingizio kuwa walifanya fujo wakati wakidai haki ya watanzania kuliona bunge live ni kitendo ambacho kinaonyesha udhaifu mkubwa kwa serikali ambayo inajinasibu kuwa inapambana na wala Rushwa na mafisadi huku ikiogopa kuweka wazi mambo yake likiwemo Bunge kuonekana na wananchi wote kama ilivyokuwa awali na ndio maana chama chake kimeamua kuzuunguka nchi nzima kwa kusirikiana na vyama vingine vya upinzani na watanzania wote kupinga hali hiyo ya ukandamizwaji wa democrasia.
Katikati ni mwenyekiti wa chama cha ACT WAZALENDO Mama ANNA ELISHA MGWIRA akiwa pamoja na katibu mkuu wa chama hicho Mh Juma Saanani pamoja na Kiongozi mkuu wa chama hicho Mh ZITTO KABWE wakifwatilia kwa ukaribu mkutano huo leo

Mh ZITTO KABWE akiwasili katika viwanja vya ZAKIEM MBAGALA jioni ya leo jumapili kwa ajili ya mkutano huo mkubwa uliomalizika jioni Hii
Mwenyekiti wa chama cha ACT WAZALENDO Mama ANNA ELISHA MGWIRA akiwahutubia mamia ya wakazi wa mkoa wa Dar es salaam katika viwanja vya mbagala Jijini Dar es salaam ambapo katika hotuba yake mwenyekiti huyo amelaani vikali kauli aliyoitoa Rais wa Jamhuri ya muungano waTanzania Dk magufuli Ya kuwaita wanafunzi waliokuwa wanasoma UDOM kuwa ni vilaza kauli ambayo amesema kama mama ambaye anaongoza kwa kujali UTU ,UADILIFU na UZALENDO kauli hiyo haifai kwa ustawi wa jamii yake na badala yake Rais awaombe Radhi wanafunzi hao na wazazi wao kwa kauli hiyo
Pamoja na kualikwa kwa vyama vingine vya upinzani vikiwemo CHADEMA,CUF na NCCR.ni chama kimoja tu kilichoweza kushiriki katika mkutano huo ambapo pichani ni kiongozi wa makamishna wa chama cha NCCR-MAGEUZI ndugu PETERSON MUSHENGERA ambaye amekiwakilisha chama chake katika mkutano huo wa hadhara.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni