.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 6 Juni 2016

WANAWAKE HUTUMIA SIKU NNE KATIKA MWAKA KUTAFUTA NGUO ZA KUVAA TU

Ni kawaida kabisa kuwaona wanawake wakipoteza muda mwingi kupekua kabati wakijaribu kufikiria nguo gani ya kuvaa kiasi hata ya kuwafanya kuwa katika hali ya kupaniki.

Watafiti wameamua kufuatili muda wanaotumia wanawake kutafuta nguo ya kuvaa na kubaini hutumia karibu dakika 17 kwa siku, sawa na siku nne kwa mwaka wakitafuta nguo kabatini.

Hali hiyo ya wanawake kutumia muda mwingi kutafuta nguo ya kuvaa kabatini hufanya moja kati ya wanawake 10 kuchelewa kazini na moja kati ya 20 hushindwa kufika kwenye hafla kabisa.

Asilimia 21 ya wanawake wamekiri kuwa kitendo cha kuhangaika kuchagua nguo ya kuvaa kabatini huwasababishia ugomvi na wenza wao.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni