.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 16 Februari 2017

GYAN NI MIONGONI WA WACHEZAJI 40 WALIONYOA NYWELE KINYUME NA MAADILI

Aliyekuwa mchezaji wa Sunderland mshambuliaji, Asamoah Gyan, ni miongoni mwa wachezaji 40, wanaoelezwa kuwa na ukataji nywele usioendana na maadili chini ya miongozo ya Chama cha Soka cha Umoja wa Nchi za Kiarabu (UAEFA).

Mchezaji huyo raia wa Ghana mwenye umri wa miaka 31 anacheza kwa mkopo huko Dubai katika Ligi ya Ghuba kwenye klabu ya Al Ahli, akitokea timu ya Shanghai SIPG.

Baadhi ya maandiko ya dini ya Kiislam yanakataza ukataji nywele kwa mitindo mbalimbali, ambapo sasa maafisa wa Umoja wa Mataifa ya Kiarabu wanataka kuzuiwa wachezaji ukataji nywele wa mitindo ili kuepusha watoto kuiga.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni