Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kyakairabwa wakimsikiliza Afisa Mahusiano na Masoko Mkuu wa TADB, Bw. Saidi Mkabakuli wakati walipotembelea Banda la TADB ili kujua shughuli za Benki hiyo kwenye Viwanja vya Kyaikarabwa yanapofanyika Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa mkoani Kagera.
Katika kuadhimisha Wiki ya Maziwa inayofanyika mjini Bukoba, wanafunzi wa Shule ya Msingi Kyakairabwa walijitokeza kwa wingi katika Banda Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ili kujua shughuli za Benki hiyo kwenye Viwanja vya Kyaikarabwa.
Wanafunzi hao walipata fursa ya kujifunza shughuli na huduma zinazotolewa na Benki hiyo.
Akizungumza na wanafunzi hao, Afisa Mahusiano na Masoko Mkuu wa TADB, Bw. Saidi Mkabakuli aliwajulisha wanafunzi hao kuwa TADB ni Taasisi ya Serikali iliyo chini ya Msajili wa Hazina na ilianzishwa kwa madhumuni makubwa mawili ambayo ni kusaidia upatikanaji wa utoshelezi na usalama wa chakula ambao ni endelevu nchini Tanzania; na kuchagiza na kusaidia Mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara ili kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini nchini.
Bw. Mkabakuli aliwaeleza kuwa Serikali iliambua kuianzisha Benki hiyo ili kutatua changamoto za ufinyu mkubwa wa upatikanaji wa fedha mikopo kwa ajili ya maendeleo ya kilimo nchini ambao unachangiwa kwa kiasi kikubwa na mikopo mingi kutoka taasisi za fedha kuelekezwa zaidi kwenye upande wa biashara za bidhaa.
Aliwatajia changamoto nyingine zilizopelekea Serikali kuianzisha TADB kuwa ni pamoja na riba kubwa kwenye mikopo ya kilimo; mikopo ya muda mfupi; masharti magumu ya kukopa bila kuzingatia hali halisi ya sekta ya kilimo na mazao ambayo inaathiriwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya hali ya hewa.
“Kutokana na changamoto hizo, Serikali iliamua kuanzisha Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ili kusaidia kukabiliana na mapungufu hayo na kuhuisha upatikanaji wa mikopo katika sekta ya kilimo ili kuleta mapinduzi katika kilimo nchini,” Bw. Mkabakuli aliwaeleza wanafunzi hao.
Katika kuwapima uelewa wao, wanafunzi hao walishindanishwa Shindano la kujua Shughuli za TADB na washindi walipatiwa zawadi mbalimbali.
Wanafunzi hao walipata fursa ya kujifunza shughuli na huduma zinazotolewa na Benki hiyo.
Akizungumza na wanafunzi hao, Afisa Mahusiano na Masoko Mkuu wa TADB, Bw. Saidi Mkabakuli aliwajulisha wanafunzi hao kuwa TADB ni Taasisi ya Serikali iliyo chini ya Msajili wa Hazina na ilianzishwa kwa madhumuni makubwa mawili ambayo ni kusaidia upatikanaji wa utoshelezi na usalama wa chakula ambao ni endelevu nchini Tanzania; na kuchagiza na kusaidia Mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara ili kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini nchini.
Bw. Mkabakuli aliwaeleza kuwa Serikali iliambua kuianzisha Benki hiyo ili kutatua changamoto za ufinyu mkubwa wa upatikanaji wa fedha mikopo kwa ajili ya maendeleo ya kilimo nchini ambao unachangiwa kwa kiasi kikubwa na mikopo mingi kutoka taasisi za fedha kuelekezwa zaidi kwenye upande wa biashara za bidhaa.
Aliwatajia changamoto nyingine zilizopelekea Serikali kuianzisha TADB kuwa ni pamoja na riba kubwa kwenye mikopo ya kilimo; mikopo ya muda mfupi; masharti magumu ya kukopa bila kuzingatia hali halisi ya sekta ya kilimo na mazao ambayo inaathiriwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya hali ya hewa.
“Kutokana na changamoto hizo, Serikali iliamua kuanzisha Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ili kusaidia kukabiliana na mapungufu hayo na kuhuisha upatikanaji wa mikopo katika sekta ya kilimo ili kuleta mapinduzi katika kilimo nchini,” Bw. Mkabakuli aliwaeleza wanafunzi hao.
Katika kuwapima uelewa wao, wanafunzi hao walishindanishwa Shindano la kujua Shughuli za TADB na washindi walipatiwa zawadi mbalimbali.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni