.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 25 Juni 2017

MAMA AKABILIWA NA MASHTAKA YA KUWAUWA WATOTO WAKE WAWILI KWA KUWAFUNGIA KWENYE GARI

Mama mmoja huko Texas Marekani anakabiliwa na mashtaka ya kusababisha vifo vya watoto wake wawili kwa joto baada ya kuwafungia kwenye gari lililoegeshwa juani mwezi uliopita.

Polisi nchini Marekani wamesema mama huyo Cynthia Marie Randolph amesema alikuwa amefanya kitendo hicho ili kumtia adabu mtoto wake wa kike wa miaka miwili aitwaye Juliet baada ya kukataa kutoka kwenye gari.

Mtoto Juliet pamoja na mdogo wake wa kiume wa miezi 16 Cavanaugh walithibitishwa kufa kwa joto na kukosa hewa Mei 26 majira ya saa kumi na nusu jioni, wakiwa kwenye joto la nyuzi joto 35.5.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni