Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (aliyevaa fulana ya kijani) akiwasili kwenye Banda la Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) lililopo kwenye Viwanja vya Ngongo, mjini Lindi.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango amelitembelea Banda la Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) wakati wa maonesho ya Nane Nane yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.
Akiwa katika Banda hilo Dkt. Mpango alionekana kuridhishwa na jitihada za Benki ya Kilimo katika kuchagiza mapinduzi ya kilimo.
Akimpokea Waziri Dkt. Mpango, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Francis Assenga alimjulisha Dkt. Mpango kuwa ndani ya Banda la TADB jumla ya washiriki 14 wanaonesha bidhaa na huduma zao kupitia Benki hiyo ikiwemo wakinamama na vijana.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni