Nyota wa Leicester City Ahmed Musa
amefungua kituo chake cha mafuta nyumbani kwao Nigeria, katika
kujiandaa na maisha baada soka.
Mchezo wa soka ni miongoni mwa kazi
ambayo mtu huifanya kwa muda mfupi kabla ya kustaafu na inaonekana
Musa kashaliona hilo na kulifanyia kazi.
Kituo hicho kiitwacho 'Myca-7'
kilichopo Kano, Nigeria kinasemekana ni cha pili kwa mshambuliaji
huyo wa Leicester kukifungua.
Ahmed Musa mwenye umri wa miaka 24,
pia anamiliki kituo cha Michezo na Mazoezi katika baadhi ya biashara
zake.
Ahmed Musa akifurahia jambo huku akimuwekea mteja wake mafuta
Hata Bajaj nazo zipo Nigeria na hapa Ahmed Musa akiweka mafuta kwenye Bajaj



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni