.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 2 Desemba 2017

BALOZI SEIF IDDI MGENI RASMI BARAZA LA MAULIDI RUANGWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa Wanawake Waislaam Tanzania, Shamim Khan baada ya kushiriki Katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likanglal wilayani Ruangwa Desemba 1, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia washiriki wa Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) baada ya kushiriki Baraza hilo kwenye uwanja wa Shukle ya Msingi Likangala wilayani Ruangwa Desemba 1, 2017.
Baadhi ya washiriki wa Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) wakimsikiliza Mgeni Rasmi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi wakati alipohutubia kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani Ruangwa Desemba 1, 2017
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akisalimiana na Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya (wapili kushoto) na kulia ni Mwenyekiti wa Wanawake Waislaam, Shamim Khan wakati alipowasili kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala kushiriki katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S. A.W). Mgeni Rasmi kaaika Baraza hilo alikuwa ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongozana na Mgeni Rasmi katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W), Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi kuingia kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani Rungwa Desemba 1, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mgeni Rasmi katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W),Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani RUangwa Desemba 1, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani Rungwa Desemba 1, 2017. Mgeni Rasmi katika Maulidi hayo alikuwa ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi.
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa (wapili kushoto) na baadhi ya Viongozi walioshiriki katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) wakimsikiliza Mgeni Rasmi Balozi Seif Ali Iddi wakati alipiwahutubia kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani Ruangwa Desemba 1, 2017. Wengine kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Wanawake Waislaam Tanzania, Shamim Khan, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Ikupa Stella Alex , Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya na Mbunge wa Viti Maalum,Hamida Muhammad Abdallah
Askofu Mkuu, Bruno Ngonyani wa Jimbo Katoliki la Lindi akizungumza katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani Ruangwa, Desemba 1, 2017. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni