.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 27 Januari 2018

ALEXIS SANCHEZ ANZA NA MAN U KWA KUWA CHACHU YA USHINDI

Alexis Sanchez ameshuka ndimbani kwa mara ya kwanza akiichezea Manchester United na kutoa pasi ya magoli mawili kati ya manne yaliyopatikana dhidi ya Yeovil kwenye mchezo wa kombe la FA mzunguko wa nne.

Mchezaji huyo wa kimataifa raia wa Chile, aliyejiunga na Manchester United akitokea Arsenal kwa kubadilishana na Henrikh Mkhitaryan jumatatu, alianza kwa kucheza pembeni kushoto katika dimba la Huish Park.

Sanchez alihusika mara kwa mara na pasi za Manchester United jana usiku na pasi yake iliyomkuta Marcus Rashford ilizaa goli katika kipindi cha kwanza na nyingine kwa Ander Herrera nayo ikazaa goli la pili kipindi cha pili.

Katika mchezo huo Jesse Lingard alifunga goli la tatu kabla ya Romelu Lukaku kufunga goli la nne katika dakika ya mwisho, na kumzawadia kocha wao Jose Mourinho mwenye miaka 55 zawadi ya siku yake ya kuzaliwa.
Marcus Rashford akifunga goli la kwanza la Manchester United baada ya kupewa pande na Sanchez
Romelu Lukaku akishangilia baada ya kufunga goli la nne katika dakika za mwisho wa mchezo huo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni