.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 1 Februari 2018

MAN UTD NA CHELSEA ZAAMBULIA VIPIGO LIGI KUU UINGEREZA

Kocha Mauricio Pochettino ameipongeza Tottenham kwa kupambana kishujaa na kupata goli ndani ya sekunde 11 la Christian Eriksen lililosaidia ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Manchester United katika dimba la Wembley.

Baada ya goli hilo Manchester United walijaribu kutaka kusawazisha huku Jesse Lingard akikosa goli, lakini Phil Jones alizamisha jahazi baada ya kujifunga la pili akitumbukiza krosi ya
Kieran Trippier.
                      Christian Eriksen akifunga goli la kwanza ndani ya sekunde 11 tu ya mchezo
Kocha Eddie Howe amesema Bournemouth imepata ushindi bora kuwahi kuupata dhidi ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Chelsea.

Bournemouth ilipata magoli yake hayo katika kipindi cha pili kupitia kwa Callum Wilson, Junior Stanislas na Nathan Ake na kuipatia timu hiyo ushindi wake wa kwanza wa ugenini katika michezo saba.
                                Nathan Ake akifunga goli la tatu lililowamaliza kabisa Chelsea

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni