.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 12 Agosti 2013

TABASAMU KIDOGO JUMATATU HII



Hii sikukuu imekuja vizuri lakini kwa wengine imewajia vibaya kabisa.

Huyu mzee akiwa chakari kwa kinywaji, yaani kalewa sawasawa, jana alipita karibu na eneo la kutupa takataka lililopo kwenye bar fulani maeneo ya Mikocheni.

Alipokuwa katika eneo lile la taka, akaona chupa mbalimbali za bia zikiwa zimetupwa eneo lile. Basi akaokota chupa tupu ya kwanza kisha akaibamiza ukutani huku akisema “ kwasababu yako nimeachana na mke wangu”

Akaokota tena chupa tupu ya pili nayo akaibamiza ukutani huku anasema “ kwasababu yako nimeshindwa kuwasomesha watoto wangu”

Akaokota chupa tupu ya tatu nayo akaibamiza ukutani huku akisema “ kwasababu yako umesababisha nikauza nyumba yangu”

Alipookota chupa ya nne, ile kuinyanyua juu akakuta ndani ina bia, yaani haijafunguliwa kama zile nyingine alizozivunja, basi akaitazama weee kisha akasema:-

“ We sina ugomvi na wewe kabisa, basi akaifungua na kuanza kunywa huku akisema, wewe huna mabaya kama hawa wenzako , wewe ni rafiki wa kweli na nakupenda sana”

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni