.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 11 Oktoba 2013

IJUMAA HIYO, ACHIA TABASAMU KAMA KAWAIDA YAKO



Hizi ndoa ngumu sana, ukiona watu wamedumu katika ndoa miaka 20 ujue wamepitia mapito mengi, lakini kikubwa wamevumiliana sana.


Mzee mmoja ambaye kila siku alikuwa haishi kugombana na mkewe, jana akiwa Brake Point Kijitonyama anapata kinywaji huku akionekana kuna jambo linamsumbua sana kichwani.


Akiwa katika hali ile ya mawazo, akachukua simu yake na mkononi na kumtumia ujumbe mfupi ( sms ) mkewe aliyekuwa nyumbani kwa muda ule.


“Vipi wife habari za saa hizi?'.


Baada ya dk 5 mkewe akamjibu:-


 “Nafa Mume wangu nafa”.


Alipousoma ule ujumbe wa mke wake, mara mume akashuka kwenye kiti cha bar na kuanza kucheza kiduku kwa furaha kubwa, kisha akaagiza mzinga mzima wa konyagi, na kutoa ofa kwa jamaa waliokuwa pembeni yake ambao hata hawajui.


Akiwa katika hali ile ya furaha huku wateja wengine pale bar wakimshangaa, mara ukaingia ujumbe mfupi kwenye simu yake.


Alipoufungua asome,akakuta umetoka kwa mkewe na unasomeka hivi:-


'Samahani mume wangu nimekutumia sms naona imekatika inasomeka NAFA, nilikuwa namaanisha  “NAFANYA USAFI HUKU JIKONI”


Mzee akaanguka chini akapoteza fahamu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni