Mwili wa Nelson Mandela ukiondolewa katika majengo ya Umoja
Picha za maandalizi ya mwisho mwisho kijijini Qunu kabla ya maziko kesho
Jeneza la Mandela jana liliondolewa kutoka katika jumba la umoja ( Union Buildings ) baada ya shughuli za kutoa heshima za mwisho kumalizika huku maelfu ya waombolezaji wengine wakikosa nafasi hiyo baada ya kusitishwa rasmi
Hata hivyo mwili wa Mandela ulisalia mjini Pretoria ambapo
usiku kucha wa kuamkia leo jumamosi kulikuwa na hafla maalum ya viongozi wa ANC nao
kutoa heshima zao za mwisho kwa Mandela katika mojawapo ya kambi za
jeshi.
Jeneza la Mandela hata hivyo lipatapelekwa kwa
ndege nyumbani kwao katika kijiji cha Qunu mkoa wa Western Cape tayari kwa mazishi ambayo yatafanyika kesho jumapili.
Mazishi ya Mandela yatakuwa kikomo cha maombolezi ambayo yamefanyika kwa siku kumi tangu afariki dunia alhamisi iliyopita ya tarehe 5 Disemba.





Hakuna maoni :
Chapisha Maoni