.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 29 Januari 2014

RAIS BARACK OBAMA AHUTUBIA TAIFA LA MAREKANI KWA MARA YA KWANZA MWAKA HUU


Rais Barack Obama wa Marekani ameahidi kutopitisha kwenye baraza la Congress baadhi ya maamuzi yake ya kukabiliana na tofauti za hali ya kiuchumi nchini mwake, katika hotuba yake aliyoitoa kwa taifa.

Katika hotuba yake hiyo ya kwanza kwa taifa la Marekani kwa mwaka huu, Rais Obama ameahidi kuchukua hatua bila kupitia chombo hicho pale inapobidi, na kutangaza nyongeza ya mishara kwa watumishi wapya wa serikali walio kwenye mikataba.

Rais Obama pia amesisitiza juu ya kuwawezesha wanawake ambapo amesema wanawake wanatoa mchango mkubwa kwa taifa la Marekani na iwapo watafanikiwa kiuchumi na taifa hilo pia litafanikiwa kiuchumi.

Pia amesisitiza kufungwa kwa gereza la Guantanamo na kumaliza kazi iliyowapeleka Afghanistan mwaka huu.

Rais Obama amegusia pia kurekebishwa kwa sheria ya kumiliki silaha kwa Wamerekani, sheria za uhamiaji, kudhibiti uchafuzi wa hewa pamoja na uzalishaji viwandani na kuongeza ajira.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni