Ligi kuu Uingereza iliendelea usiku wa kuamkia leo kwa Arsenal kuwakaribisha Emirate Stadium Manchester United katika pambano ambalo lilimalizika kwa timu hizo kugawana pointi moja moja baada ya kushindwa kufungana.
Arsenal walikuwa na nafasi nzuri ya kuibuka na ushindi lakini mshambuliaji wake Olivier Giroud alishindwa kutumia vizuri nafasi aliyoipata alipokuwa amebaki yeye na mlinda mlango wa Man U.
Kwa matokeo hayo, Arsenal wapo nafasi ya pili na pointi 56 na Manchester United wanaendelea kubaki nafasi ya saba na pointi 42
Olivier Giroud aliposhindwa kufunga baada ya kubaki yeye na kipa tu
Van Persie akijaribu bila mafanikio kutikisa nyavu za Arsenal
LIVERPOOL YASHINDA: YAICHAPA FULHAM 3-2
Nahodha wa Liverpool Steven Gerald akifungia timu yake bao la kwanza kwa mkwaju wa penati dhidi ya Fulham
Mchezaji wa Liverpool Daniel Sturridge akichezewa madhambi ndani ya 18
Mlinda mlango wa Fulham akiwa ameumia usoni baada ya kugongana na Suarez
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)








Hakuna maoni :
Chapisha Maoni