Polisi nchini
Uganda wamezuia maandamano ya wanawake waliokuwa wakiandamana katika
Mitaa ya Jiji la Kampala kupinga sheria mpya inayowakataza wanawake
kuvaa vimini.
Badala yake
wanawake hao wapatao 200, ambao baadhi yao walikuwa wamevaa vimini,
walikusanyika kwenye jengo la makumbusho ya taifa na kupaza sauti zao
za kukerwa na sheria hiyo.
Kumekuwepo na
matukio kadhaa katika wiki za hivi karibuni ya wanawake waliovaa
sketi fupi kubughudhiwa mitaani na wanaume pamoja na kudhalilishwa
tangu kusainiwa kwa sheria hiyo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni