.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 15 Machi 2014

JENGO LA GHOROFA 17 LINALOFANANA NA MTI KUJENGWA MWAKANI NCHINI UFARANSA

Jengo la ghorofa 17 ambalo linafanana na mti linatarajiwa kujengwa huko Montpellier nchini Ufaransa, kuanzia mwakani.
 
Jengo hilo la makazi litajulikana kama “The White Tree” ama kwa lugha ya Kiswahili Mti Mweupe, litakuwa na umbo mithili ya matawi yanayotoa kivuli na kuvuta mwanga kuingia ndani yake.
Kazi ya usanifu wa jengo hilo imefanywa na msanifu Mfaransa na Wajapani litakuwa na baa kwa juu, hoteli na sehemu ya sanaa za michoro, huku watu wakipata kuona vyema mlima na bahari.

Pia litakuwa na nyumba za makazi 120, zenye vyumba na muondo wa aina tofauti kulingana na mahitaji ya familia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni