Usiku wa leo kulikuwa michezo mingi tu ya kimataifa ya kirafiki iliyopo katika kalenda ya Fifa, ambapo katika michezo hiyo Ujerumamani imeifunga Chile bao 1-0, bao ambalo liliwekwa kimiani na Mario Gotze ( pichani juu ) baada ya kupokea pasi safi toka kwa Mesut Ozil
Mesut Ozil akimiliki mpira mbele ya mchezaji wa Chile
Kwinginenko Uingereza ilifanikiwa kuifunga Denmark bao 1-0, bao ambalo lilifungwa na Daniel Sturridge
Yenyewe Poland iliifunga Scotland bao 1-0, bao ambalo lilifungwa na Scott Brown ( pichani juu )
Mashabiki wakifuatilia mchezo huo wa Poland na Scotland
Mechi nyingine ilizikutanisha Ireland na Serbia, mchezo uliomalizika kwa Ireland kufungwa na Serbia mabao 2-1
Mjini Soweto Afrika kusini ilikuwa na siku mbaya nyumbani kwao baada ya kukubali kipigo kikali cha mabao 5-0 toka kwa Brazil ambao ni wenyeji wa kombe la Dunia mwaka huu. Mabao ya Brazili yalifungwa na Neymar ambae alifunga mabao 3 katika mguu wake mwenyewe, huku Oscar na Fernandinho wakifunga bao moja moja
Furaha ya kuitandika Afrika Kusini 5-0
Mshambuliaji wa Wales, Gareth Bale jana aliisadia nchi yake kuifunga Iceland mabao 3-1 katika mchezo mwingine wa kimataifa wa kirafiki
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)












Hakuna maoni :
Chapisha Maoni